WACHEZAJI NYOTA WA EVERTON WASHINDANA KUPIKA CHAKULA CHA ASILI CHA KITANZANIA
NA MARIAMU MTORO
. Timu mbili za wapishi zilizoundwa na Phil Jagielka na Dominic Calvert-Lewin na nyingine ya kina Davy Klaassen na Matty Pennington zilichuana kuonyesha umahili wa kupika chakula cha asili cha Kitanzania.
Timu hizo zilishindana kupika
chalula cha kiasili cha Tanzania ambapo Jagielka na Lewin walitakiwa
kupika ugali na waliaanza kwa kukoroga uji kisha kupika ugali huo wakati
Davy na Matty walipewa kazi ya kupika ndizi na nyama.
Wakisaidiwa
na Mpishi Mkuu wa Hoteli ya Sea cliff, aliyetambulika kwa jina Niko
nyota hao walijifunza kuhusu upishi wa chakula cha asili cha Watanzania
ambacho walisifikia kuwa ni kitamu na baadaye kikaonjwa na balozi wa
timu yao, Graham Stuart ambaye ndiye alimtangaza mshindi.

Comments
Post a Comment