Posts

Showing posts from July, 2017

KIUNGNO MWENGINE WA RASTA ASINI

Image
                                                            WAKATI kiungo rasta, Tshishimbi Kabamba ‘Papii’ akisaini mkataba wa miaka miwili kuitumia Yanga, mabosi wa klabu hiyo wamefanya kitu kingine cha maana baada ya kumalizana na kiungo mwingine fundi. Yanga imemsainisha kiungo Raphael Daud kutoka Mbeya City tayari kuitumikia klabu hiyo na leo Ijumaa timu inatarajiwa kutua kambini mjini Morogoro kuungana na wachezaji wenzao kwa maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Habari kutoka kwa mabosi wa Yanga, ni kwamba Rafael alisainishwa mkataba huo juzi Jumatano, lakini waliamua kufanya siri kwa sababu kuna mambo hawajamalizana na klabu yake ya City. “Rasta amesaini tayari kuanza kuitumikia Yanga, lakini pia tumemalizana na kiungo Rafael Daud ambaye tulishaanza mazungumzo naye mapema, lakini ikawa bado kusaini ...

WASAJILIWA WA YANGA NI WA KIMATAIFA ZAIDI.

Image
                    Mwenyekıtı wa kamati ya usajili wa tımu ya yanga HUSSENI NYIKA amesema kuwa usajılı wa tımu yake nı wakımataıfa kulıngana na wachezajı wao walıowasajili kuwa ni wa vıwango vya kımataifa amesema amesajıli madhubutı ıli kujua wanafnya vrzri kımataifa.                                                                Waliosajıriwa nı Ibrahimu Ajibu. Abdallah Shaıbu. Ibrahımu Yahaya. Donald Ngoma. Thabanı kamusoko. Nyıka amesema wamefıkia usajili wao kwa asilimia 95%. Pamoja na hayo amesema kuwa wapochezajı walio mwagwa kuwa ni Raphel Daudai Mbeya city.                                                             ...

''OJ'' OSCAR JOSHUA CINA KINYONGO NA YANGA

Image
 Aliekuwa beki  kushoto Oscar Joshua mwenye mwılı kaa Jumba ameondoka Yanga akıwa hana kınyongo na tımu .Amesema ataendlea kuıkumbuka Yanga katika maisha kwanı imeweza kumsaidia kımaisha kufikia hapo alipo cına kinyongo na yanga kwanı maısha ndıvo yalivyo.  Mchezajı huyo amesaema kuwa yanga kuachwa kwakwe katıka msımuu huu hakutamnfnya aache kuıkumbuka yanga kwanı ımemfanya aweze kucheza  kıımataıfa na taıfa kwa ujumla xaxa kanajıpanga kuibuka kiivıngıne.        “Yanga, ina watu tofauti na wenye kazi tofauti, nilikuwa makini kutumia nafasi hizo ili kujifunza mengi yenye faida kwa maisha yangu, sitaacha kuishukuru na kuachwa kwangu hakuwezi kujenga uhasama nao,” alisema Oscar ‘OJ’  Ijulikane kuwa waliosajiriwa yanga wanahıtajı kujıtuma.

MAZOEZI YA YANGA YAANZA WAKIWA NA NYOTA WAAPYA

Image
                                 Dar es Salaam.Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeanza mazoezi ya uwanjani, ikiwa na nyota wake wapya wakiwamo Mkameruni, Fernando Bongyang na Mnigeria Henry Tony Okoh walipiga mpira mwingi, huku Kiberenge Burhan, Yahya Akilimali akifunika zaidi. Mazoezi hayo yalifanyika jana asubuhi kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam chini ya Kocha George Lwandamina na wasaidizi wake, ambapo asilimia kubwa ya wachezaji waliosajili na timu hiyo na wale wa zamani walishiriki. Kipa Youthe Rostand, Ibrahim Ajib, Akilimali na nyota hao wa kigeni wanaowania nafasi moja iliyosalia walionyesha uwezo wao, japo kiungo rasta kutoka Swaziland, Tshishimbi Kabamba 'Papii' hakuwepo kabisa uwanjani hapo. Kocha Lwandamina alisema ameanza vizuri kuwaona vijana wake na anaimani ataendelea kuwasoma kadri wakiendelea kujifua baada ya kutumia wiki mbili na ushei kwenye ma...

KESSY APATA PRESSURE YA MAJINA MAKUBWA KIKOSINI ''SAPRAIZID''

Image
                       BEKI wa Yanga, Hassan Kessy, ametamka kauli ya kishujaa kwamba mechi ya Ngao ya Jamii itakayopigwa Agosti 23 kati yao na Simba ni nyepesi sana, ila kinacholeta presha ni sapraizi ya majina makubwa ya mastaa waliosajili kikosini. Kessy aliyenyakuliwa kitatanishi toka Simba, alisema ujio wa nyota wapya Yanga umeongeza presha kikosini, lakini hiyo ni dalili njema za Yanga kutisha msimu huu. “Kuna tofauti ya ugumu wa mechi na majina makubwa ya wachezaji, mfano mzuri ni uhamisho wa Ibrahim Ajibu kutoka Simba kuja Yanga, hilo linaibua presha kwa mashabiki kuona kama kuna kitu cha ajabu kinakuja wakati soka ni lile lile,” alisema Kessy. Kuhusu mechi hiyo ya Ngao ya Jamii, alisema haoni cha ajabu katika mechi hiyo zaidi ya mchezaji kuzingatia majukumu yake uwanjani na kutovunja sheria za soka kwa maana ya mashabiki kupata burudani inayotakiwa. “Mtu kama Emmanuel Okwi ni mchezaji gani asiyemjua...

MRITHI SAHIHI WA CHUJI APATIKANA YANGA

Image
Hakuna shaka juu ya hilo.Athuman Idd Chuji alikuwa mchezaji mahiri enzi zake.Akicheza kama kiungo mkabaji,alionyesha uwezo wake na kuwa tishio kwa timu pinzania,Si hapa nchini tu bali pia aliogopwa na kusifiwa hadi nje ya nchi, Lakini tangu alipoondoka yanga,Timu hiyo imeshindwa kumpata mrithi wa kuchukua nafasi yake.Wamejaribiwa wengi lakini hakuna aliyeonyesha au kuukaribia uwezo wa Chuji. Anaitwa Papi Kabamba Tshishimbi .Alikuwa mchezaji wa Mbabane Swallows na alikuja Tanzania kwa mara ya kwanza na timu yake kuvaana na Azam kwenye mchezo wa kwanza wa mtoano wa Kombe la shirikisho.Kiwango chake kilimvutia kocha George Lwandamina na akaamua kumuwekea mashushushu wa kujua ni nani hasa mchezaji huyu.Lwandamina mwenyewe alifika hadi Swaziland kumshuhudia mchezaji huyu katika moja ya mechi alizocheza akiwa na Mbabane Swallows...akaridhika nae. Ni jana tu ,jamaa huyu akatia timu Tanzania kimya kimya na kuanza mazungumzo na uongozi wa Yanga,Mda si mrefu atatambulishwa na kwa ai...

:DOCTOR; SALVATORY EDWARD AENDLEA KUDUMISHA UMOJA NA USHIRIKIANO YANGA.

Image
                                        Kungo mshambulıajı wa Tımu ya Yanga Salvatoyr Edward DOCTOR aendlea kuudımısha umoja na ushırıkaıno kwa vıjana wake alokuwa anawafundısha akıwa kocha wa Yanga . Salvatory kaıchezea yanga mwaka 1990 na kupata mafunıkıo hadı mwaka 2000. Ameendlea kuwapokea vıjana hao na kuwapa nafası amewaongoza vıjana wake jana kucheza mechı ya kırafıkı ya Lıpulı FC kwenye uwanja wa Karume.                   kocha huyo amesema mbalı na kuwapeleka vıjana hao kwenye mechı tofautı tofautı pıa anaendlea kuwauza kweny tımu kubwa ılı waje wacheze kweny lıgıı kuu bara.                Lıpulı fc ınatarajıwa kukarıbıshwa kwnye msımuu huu wa lıgı kuu Tanzanıa Bara 2017/ 2018 na kuaanza kucheza na bıngwa mtetezı Yanga wa lıgıı kuu agostı 27.

KICHUYA HADI KIELEWEKE MIMI NA YANGA

Image
                                                                                    MASHABIKI na wachezaji wa Yanga, huenda bado wanaendelea kumuota Shiza Kichuya kwa jinsi mabao yake mawili yalivyowakata maini katika mechi ya watani msimu uliopita, lakini kama wanadhani watapumua, wamsikie anachokisema. Kichuya aliyesajiliwa Simba kutoka Mtibwa Sugar, ndiye aliyefunga bao la kusawazisha katika mechi iliyojaa utata ya Oktoba Mosi, 2016 kabla ya kufunga bao la ushindi mechi ya marudiano na kuwazima kabisa Yanga, alisema yupo tayari kufanya yake. Winga huyo aliyepo timu ya taifa, Taifa Stars, ambayo kesho Jumamosi itashuka Uwanja wa Amahoro mjini Kigali kucheza mechi ya marudiano ya kufuzu fainali za Chan 2018 dhidi ya wenyeji Rwanda, alisema Yanga haimpi shida kwa vile ...

JEERY MURO AJITOA YANGA

Image
                                                  Aliyekuwa msemaji mkuu wa klabu yanga amesema kuwa Yang ilikufanikiwa katika utendaji ndani ya uongozi wa mabingwa hao wa kihistoria ni lazima kuangalia ni nani anakuletea ushauri. Muro ameyasema hayo ikiwa ni sikuchache tu zimepita tangu Yanga imtangaze msemaji mpya wa timu hiyo, Dismass Ten aliyochukua nafasi yake. “Yanga kuna majungu watu wanapenda wafanye vitu vyao, kuna wanafiki ambao watakwambia ufanye hiki ukikifanya unaingia chaka. “Wapo Yanga SC watu wenye msaada wa kweli, wazuri sana, wenye akili na wenye mapenzi ya kweli kuhakikisha Yanga inakuwa kama    watu wote hao wapo Yanga. “Unachotakiwa kufanya ni kufungua macho kuangalia ni nani anakuletea ushauri, maana kuna mwingine anakuletea ushauri wakati yeye kashindwa kuongoza nyumba yake kaachana na mkewe ,hajali wa...

SIMBA YASAJILI WALINZI KUMI NA NNE (14) KUMZUIA AJIBU

Image
                                         ;KIBERENGE AFURAHI KUCHEZA NA AJIBU            Jana mchana mabosi wa Yanga walimalizana na Burhan Yahya Akilimali aliyedakwa juu kwa juu wakati akiwania kusajiliwa Lipuli na kumsainisha mkataba wa miaka miwili. Yahya anayekwenda kwa jina la utani la Kiberenge kutokana na kasi aliyonayo, ametua Jangwani kuchukua nafasi ya Simon Msuva anayejiandaa kutimkia Morocco na amesema anajisikia furaha kutua timu kubwa yenye nyota kama Ajibu, Tambwe na Ngoma na kuahidi kutowaangusha.                                                                                               ...

FURAHA YANGA YAMPATA KAMUSOKO NA KAMBWILI KIPA WA SERENGETI BOY.

Image
                                                                    Klabu ya Yanga imemsainisha mkataba mpya wa miaka miwili kiungo Mzimbabwe, Thaban Kamusoko huku pia ikimsajili kipa wa Serengeti Boys, Ramadhani Kabwili. Taarifa iliyotolewa na Yanga kupitia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika ni kwamba Kamusoko ameongeza mkataba huo baada ya kufikia makubaliano ya mambo kadhaa. Katika kuimarisha lango lao, Yanga pia imefanya usajili wa Kabwili ambaye alikuwa na Serengeti Boys katika michuano ya Vijana Afrika mwaka huu nchini Gabon. Usajili umeifanya Yanga kukamilisha usajili wa nyota wanne wapya ambapo awali ilimsainisha kipa wa African Lyon, Youthe Rostand, beki Abdallah Shaibu pamoja na mshambuliaji Ibrahim Ajib.

WAKILII DAMASI NDUMARO YAFUTIWA KESI NA TFF

Image
                               Shirikisho la soka nchini Tanzania  (TFF)  limetangaza kumfutia kifungo cha kutojihusisha na masuala ya soka wakili   Damas Ndumaro   ambaye alifungiwa kwa muda wa miaka saba. Maamuzi hayo yamechukuliwa na Kamati ya rufaa ya TFF    chini ya mwenyekiti wake, Rahim Shaban Zuberi ambaye ndiye aliyetangaza maamuzi hayo kwenye ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam, leo Jumatano. Hadi anafikia hatua ya kufunguliwa, Ndumbaro alikuwa ametumikia adhabu yake kwa muda wa miaka miwili na nusu. Katika maelezo yake, Zuberi amesema Ndumbaro hakupata nafasi ya kujitetea na kuna badhi ya mambo hayakuzingatia usawa wakati akifungiwa.

UPINZANI HAKUNA UCHAGUZI WA TFF.

Image
                                Arusha. Katibu mkuu wa zamani wa Chama cha Soka Mkoa wa Arusha (ARFA), Adam Brown ameeleza kuwa uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania unaotarajia kufanyika mwezi ujao  Dodoma utakuwa rahisi kuliko miaka iliyopita. Mkongwe huyo aliyewahi kuwa meneja wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ mwaka 2001, alisema hali hiyo ni kutokana na wengi wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi TFF hawajaweka mizizi kwa kiasi kikubwa kwenye familia ya wanamichezo kama ilivyokuwa kwa wagombea wa miaka ya nyuma. Alisema miaka ya nyuma mtu mwenye nia ya kuwa kiongozi katika shirikisho hilo alikuwa anatambulika mapema kwa matendo yake ya kujihusisha na masuala ya maendeleo ya soka kuanzia mikoani hadi taifa.

TASMA (Uchaguzi wa chama cha wataalamu wa Tiba za Michezo),YAWEKA WAZI MAJINA YA WALOCHUKUWA FOMU

Image
                          Dar es Salaam. Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Wataalamu wa Tiba za Michezo (TASMA), kimetangaza majina ya waliochukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Agosti 5, mwaka huu. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya chama hicho, Leslie Liunda alisema wanaowania uenyekiti ni Joakim Mshanga, Usubene Kisongo na Biyondo Mgome ilihali kwenye nafasi ya Makamu Mwenyekiti, amejitokeza Magreth Mtaki pekee. anaotaka ukatibu mkuu wa chama hicho ni Suphian Juma na Nassoro Matuzya waliojitokeza huku nafasi ya ukatibu msaidizi inawaniwa na Alfred Mchinamnamba. Nafasi Mweka Hazina inawaniwa Alex Gongwa huku Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF inawaniwa Richard Yomba na Cosmas Kapinga ilihali Ujumbe wa Kamati ya Utendaji wamo   Paschal Itonge na Mwanandi Mwankemwa. Kwa mujibu wa ratiba ya mchakato wa uchaguzi huo kuanza leo na kesho (Jul...

IBRAHIMU AJIBU NA ABDULRAHMAN MUSSA WALILIWA TAIFA STAR

Image
                                Taifa  Stars chini ya Kocha Salum Mayanga, imeonekana kuwa na tatizo katika safu yake ya ushambuliaji, lakini kitu cha ajabu nje ya kikosi hicho kuna mastraika tishio kwa kucheka na nyavu, Ibrahim Ajibu na Abdulrahman Mussa.                                                                                                                 Mussa anayeichezea Ruvu Shooting alimaliza msimu uliopita akiwa na mabao 14 huku Ajibu aliyepo Yanga kwa sasa alikuwa na mabao manane akiichezea Simba na kuisaidia kuiweka kwenye mbio za ubingwa, lakini wote wameachwa kwenye kikosi cha timu ...

ROONEY KUIKABILI GOR MAHIA

Image
NA MARIMU MTORO Mshambuliaji Wayne Rooney atacheza mechi yake ya kwanza akiwa na kikosi cha Everton leo dhidi ya Gor Mahia kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam (saa 11:00 jioni). Rooney atacheza mechi hiyo ya kwanza tangu alipoiacha klabu hiyo ya Merseyside mwaka 2004, pia winga Aaron Lennon atacheza mchezo  huo baada ya kupona ugonjwa wake wa msongo wa mawazo. Rooney atakiongoza kikosi hicho cha kocha Ronald Koeman kuhakisha kinatoka na ushindi dhidi ya Gor Mahia mabingwa wa Kombe la SportPesa. Rooney amepokelewa kwa shangwa tangu alipoamua kurejea Goodison Park na atacheza mechi hiyo ya kwanza akiwa na jezi ya Blues tangu alipofanya hivyo Mei 2004. Nahodha huyo wa zamani wa England, alifanya mazoezi na kikosi hicho jana Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa. Pamoja na mashabiki wa Afrika Mashariki kuwa na wasiwasi kwamba Gor Mahia itachapwa mabao mengi, wenyewe wamesema watawaduwaza wengi.  Beki wa Gor Mahia, Harun Shakava amesema  wanauchukuli...

SINGIDA UNITED YAKANA KUTAKA KUSAJILI WACHEZAJI TOKA YANGA

Image
DIDA NA BARTHEZ NA MARIAMU MTORO Klabu ya Singida United, imesema haina mpango wa kuwasajili wachezaji watatu kutoka Yanga kama inavyodaiwa. Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu uliopita inahusishwa na kutaka kuwasajili makipa wawili wa Yanga, Deogratius Munishi 'Dida’ na Ally Mustapha ‘Barthez’ pamoja na beki Oscar Joshua. Katibu mkuu wa Singida United, Abuurahman Sima amekana taarifa hizo kwa kusema timu hiyo haina mpango na wachezaji hao.  “Hizo ni tetesi tu ambazo ni wakati wake ila kwenye uongozi wetu bado hakuna taarifa za timu yetu kumtaka huyo beki {Joshua} wala kipa yeyote kutoka Yanga kwa wakati huu,” alisema Sima.

YANGA KUKAMILISHA USAJILI BAAB KUBWA WIKI HII

Image
                                                                                                                                                                      ...

WACHEZAJI NYOTA WA EVERTON WASHINDANA KUPIKA CHAKULA CHA ASILI CHA KITANZANIA

Image
NA MARIAMU MTORO .  Timu mbili za wapishi zilizoundwa na Phil Jagielka na Dominic Calvert-Lewin na nyingine ya kina Davy Klaassen na Matty Pennington zilichuana kuonyesha umahili wa kupika chakula cha asili cha Kitanzania. Timu hizo zilishindana kupika chalula cha kiasili cha Tanzania ambapo Jagielka na Lewin walitakiwa kupika ugali na waliaanza kwa kukoroga uji kisha kupika ugali huo wakati Davy na Matty walipewa kazi ya kupika ndizi na nyama. Wakisaidiwa na Mpishi Mkuu wa Hoteli ya Sea cliff, aliyetambulika kwa jina Niko nyota hao walijifunza kuhusu upishi wa chakula cha asili cha Watanzania ambacho walisifikia kuwa ni kitamu na baadaye kikaonjwa na balozi wa timu yao, Graham Stuart ambaye ndiye alimtangaza mshindi.

TUJIKUMBUSHE MECHI KALI KATI YA YANGA NA SIMBA NYAMAGANA 1974?

Image
Kikosi cha Yanga cha mwaka 1973 kabla Dk. Victor Stanculescu (wa pili kushoto) hajaondoka. Anayeongea na wachezaji na meneja wa timu, Shiraz Sharrif. Wengine ni Hassan Gobbos, Kitwana Manara, Maulid Dilunga, Sunday Manara, Elias Michael, Boi Idd 'Wickens', Selemani Said, Gibson Sembuli, Omar Kapera, Ally Yussuf, Abdulrahman Juma (nahodha). NA MWANDISHI WETU KWA wenye kumbukumbu nzuri bila shaka kipigo cha Nigeria cha magoli 2-1 toka kwa Italia katika raundi ya pili ya Kombe la Dunia huko Marekani mwaka 1994 kiliwarudisha mapema miaka ya 1970 pale Yanga ilipoichapa Simba magoli 2-1 kwenye fainali ya Ligi ya Taifa ya Soka kwenye Uwanja wa Nyamagana, Mwanza. Nasema huenda kumbukumbu hiyo ikawa imejitokeza kufuatia kufanana kwa kiasi kikubwa kwa matokeo hayo, hasa muda, yaani ‘timing’, magoli hayo yalipopatikana. Katika mchezo wa Nigeria na Italia Alhamisi ya Julai 14, 1994, Nigeria ilikuwa ikiongoza kwa goli moja ililolipata mapema kunako dakika ya 26 hadi dakika ya 87 Rob...

DUA SAID ALIVYOWADUWAZA YANGA 1993

Image
LIGI Kuu ya Muungano iliyosadikiwa kuwa na msisimko wa kipekee msimu huo kwa vile ilikuwa inawahusisha kikamilifu mamilionea wote watano waliokuwa wanafadhili soka nchini Tanzania, ilianza rasmi Jumamosi Septemba 25, mwaka huo 1993 na ilitarajiwa kupamba moto zaidi Jumapili katika kindumbwendumbwe cha aina yake kwa kuzikutanisha Simba na Yanga. Siku hiyo ya Jumamosi Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora ulianza ukurasa mpya wa kumbukumbu zake kwa mechi za Ligi Kuu ya Muungano kuchezewa kwenye nyasi zake. Abbas Gulamali, Murtaza Dewji, Azim Dewji, Mohammed Raza na Naushad Mohammed, wafanyabiashara wa Tanzania wenye asili ya Asia, ambao walikuwa wamebobea katika kutumia utajiri wao kuzifadhili timu kubwa nchini, walitarajiwa kuonyesha ubabe katika ligi hiyo na mwenzao Salim Kanji alikuwa anakabiliwa na upinzani mkali. Hivyo, ligi hiyo ilitazamiwa kutegemea zaidi mbinu za midani kuliko kiwango cha soka. Naushad wa Malindi Jumamosi hiyo alikuwa anamkabili Kanji wa Milambo huko...

JINSI KOCHA WA YANGA TAMBWE LEYA, ALIVYOMUIBUA NONDA SHAABAN PAPII

Image
Yanga Yosso ya mwaka 1995. Kutoka kushoto waliosimama kipa Mahmoud Nyalusi, Reuben Mgaza, Nonda Shaaban 'Papii', Sylvatus Ibtahim 'Polisi', Ally Yussuf 'Tigana', Sammy Bitumba Iyela, James Tungaraza na kipa Sadiq Kalokola na kiongozi wa Yanga. Waliochuchumaa kutoka kushoto Mzee Abdallah Ngauja, Bakari Malima 'Jembe Ulaya', Stephen Nyenge, David Mjanja, Mohammed Hussein Daima 'Mmachinga', Salvatory Edward na Benny Luoga Kikosi cha Yanga (Yosso) cha mwaka 1995. Kutoka kushoto waliosimama ni meneja wa timu Nurdin, kipa Mahmoud Nyalusi, Kenneth Mkapa, Reuben Mgaza, Sylvatus Ibtahim 'Polisi', Dominic Mbawala, Ally Jabir Katundu, Sadiq Kalokola, kocha mkuu Tambwe Leya, kocha msaidizi Nzoysabah Tauzany. Waliochuchumaa ni Maalim Salehe 'Romario' James Tungaraza 'Boli Zozo', Ally Yussuf 'Tigana', Anwar Awadh Gessan, Mzee Abdallah Ngauja, Mohammed Hussein Daima 'Mmachinga' na Bakari Malima 'Jembe Ulaya HI...