KICHUYA HADI KIELEWEKE MIMI NA YANGA
Kichuya aliyesajiliwa Simba kutoka Mtibwa Sugar, ndiye aliyefunga bao la kusawazisha katika mechi iliyojaa utata ya Oktoba Mosi, 2016 kabla ya kufunga bao la ushindi mechi ya marudiano na kuwazima kabisa Yanga, alisema yupo tayari kufanya yake.
Winga huyo aliyepo timu ya taifa, Taifa Stars, ambayo kesho Jumamosi itashuka Uwanja wa Amahoro mjini Kigali kucheza mechi ya marudiano ya kufuzu fainali za Chan 2018 dhidi ya wenyeji Rwanda, alisema Yanga haimpi shida kwa vile anajiamini.
Kichuya alisema anafahamu Yanga watakuwa wakimpangia mikakati kuelekea mechi ya Ngao ya Jamii itakayopigwa Agosti 23, sambamba na ile ya Ligi Kuu Bara Oktoba 14, lakini anaendelea kujiweka sawa ili kuisaidia timu yake.

Comments
Post a Comment