Posts

Showing posts from September, 2017

LIGI KUU BARA...WACHEZAJI MAHIRI KUPIGA MIPIRA YA ADHABU NDOGO

Image
                       Ibrahim Ajibu |  Amekuwa akifunga magoli ya mipira ya adhabu mara kwa mara tangu akiwa Simba, msimu huu tayari amesha fanya hivyo dhidi ya Njombe Mji                   Thaban Kamusoko |  Tangu ajiunge na Yanga misimu mitatu nyuma amekuwa ndiye mpigaji maalumu wa mipira ya adhabu, Hajawahi kufanya kosa                 Shiza Kichuya |  Amejizolea umaarufu katika kipengele cha kupiga mipira ya adhabu maarufu kama "Kichuya Kona".                   Emmanuel Okwi |  Ni mara ya tatu anarudi kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara, awamu moja Yanga na hii ni ya tatu kwa Simba, msimu huu bado hajaonyesha cheche zake, lakini anak...

NATAKA KUFUNDISHA YANGA

Image
Nahodha wa Yanga Nadiri Haroub amesema hachukii maamuzi ya kocha wake George Lwandamina kumuweka benchi na zaidi anajifunza ili kuja kuwa kocha    Nahodha wa Yanga Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema atakapostaafu kucheza soka anataka kusomea ukocha ili kuja kuchukua mikoba ya kocha wake wa sasa George Lwandamina. Cannavaro licha ya kuwa na cheo hicho lakini amekuwa hapati nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza kutokana na umri wake kumtupa mkono. “Hata kama sichezi lakini nafurahi kuwa benchi kwasababu najifunza mambo mengi kutoka kwa makocha waliopo na lengo langu baada ya kustaafu kucheza nataka kuja kuifundisha Yanga siku zijazo,” amesema Cannavaro. Nahodha huyo ameiambia YOUNGA AFRICAN ,  hakuna kinachoshindikana katika hilo kwani kwakipindi cha misimu 11, alichoitumikia Yanga ameweza kujifundisha mambo mengi kutoka kwa makocha mbalimbali ambao wamepitia timu hiyo. Mkongwe huyo amesema mipango yake baada ya kustaafu kucheza soka ni kwenda...

AJIBU AANZA KUTIMIZA WAJIBU

Image
        Pamoja na ushindani mkali lakini mabingwa watetezi wa taji la Ligi Kuu ya Tanzania Bara Yanga ,wameonja ladha ya ushindi kwa kuifunga Njombe Mji    Mshambiliaji wa zamani wa Simba Ibrahim Ajibu leo ameipa pointi tatu klabu yake mpya ya Yanga baada ya kufunga bao pekee lililoipa timu hiyo pointi tatu walipokuwa wanacheza ugenini dhidi ya Njombe Mji ya Ruvuma. Bao hilo limeifanya Yanga kufikisha pointi nne sawa na timu ya Simba, lakini mabingwa hao wapo kwenye nafasi ya tano kwenye msimamo huku Simba wakiongoza ligi hiyo kwa tofauti ya mabao. Ajibu alifunga bao hilo mapema dakika ya 16, akipiga mpira wa adhabu ndogo uliompita kipa wa Njombe Mji David Kisu na mpira kujaa wavuni. Wenyeji Njombe Mji ndio waliouanza mchezo huo kwa kasi lakini baada ya dakika tano walijikuta wakikaribisha mashambulizi ya Yanga kwenye lango lao na kufungwa bao hilo ambalo lilidumu kwa muda wote wa mchezo. Mshambuliaji wa Yanga Donald ...

NATISHA SABABU YA KOCHA WANGU-MSUVA

Image
Msuva amesema kiwango chake bora alichokionyesha  dhidi ya Botswana, kimetokana na juhudi binafsi ambazo amezionyesha tangu kujiunga na Difaal    Mshambuliai wa Difaal El Jadida ya Morocco, Simon Msuva, amesema siri ya kufanya kwake vizuri ni kutokana na mbinu alizopewa na kocha wake Bderrahim Taleb, anayeifundisha timu hiyo aliyojiunga nayo hivi karibuni akitokea Yanga. Msuva ameiambia YOUNGA AFRICAN , kwa muda mfupi alioichezea timu hiyo ameweza kujifunza mengi ikiwemo mbinu za kuwatoroka na mabeki na kufunga mabao kama aliyofunga jana na kuipa ushindi wa mabao 2-0 Tanzania. “Naweza kusema bado kuna mambo mazuri zaidi yanakuja kutoka kwangu kwani huu ndiyo mwanzo hata ligi haijaanza lakini nimekuwa na mwanzo mzuri ambao mpaka sasa miweza kufunga mabao 9 katika mechi 12 za kirafiki nilizocheza,”amesema Msuva. Mshambuliaji huyo wa pembeni pia amemshukuru kocha Salum Mayanga kwa kumuita kwenye kikosichake na kumpa nafasi ya kucheza hata k...

TAMBWE NA CHIRWA KUISUBIRI SIMBA

Image
Kocha wa Yanga George Lwandamina amewaondoa kwenye kikosi chake kitakacho kwenda Kusini wacheza Tambwe na Chirwa ili wapone vizuri majeraha yao    Kocha George Lwandamina wa Yanga amewaondoa wachezaji, Obrey Chirwa na Amissi Tambwe, kwenye kikosi kitakacho kwenda Nyanda za Juu Kusini kwa ajili ya mechi mbili za ligi dhidi ya Njombe Mji na Majimaji FC. Lwandamina ameiambia YOUNGA AFRICAN , kuwa analazimika kuwaacha wachezaji hao ili waweze kupona vizuri na atawatumia kuanzia mchezo dhidi ya Ndanda FC, ambao utapigwa Dar es Salaam Septemba 23 na ule dhdi ya Mtibwa Sugar ambao utapigwa Septemba 30. “Wanakosa fitness ndiyo maana nataka kuwapumzisha ili wafanye mazoezi kwa muda mrefu zaidi lengo ni kuwaanda kwa ajili ya mechi hizo na nyingine ambazo tutakwenda kucheza kanda ya Ziwa kabla ya kupambana na Simba Oktoba 28,”amesema Lwandamina. Kocha huyo raia wa Zambia amesema maandalizi yao yanakwenda vizuri kuhakikisha wanashinda mechi hizo mbili amba...

AZAM FC YAFURAHIA MECHI ZAKE NA YANGA KUPELEKWA CHAMANZI

Image
Mabadiliko ya ratiba mpya ya Ligi Kuu yanaonyesha kuwa mechi zote za Azam FC za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zitafanyika Uwanja wa Azam Complex.   Klabu ya Azam FC imefuraishwa na taarifa za shirikisho la mpira TFF kuruhusu mechi zao dhidi ya  Simba na Yanga kufanyika kwenye uwanja wao wa Chamanzi. Kwa mara ya kwanza mechi ya Azam na Simba itafanyika katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Jumamosi hii Septemba 9. " Ni furaha tupu ndani ya viunga vya Azam Complex kwenye makao makuu ya Klabu BIngwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuiruhusu timu hiyo kutumia uwanja huo kwa mara ya kwanza kwenye mechi zake za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga. waliandika hivyo kupitia kwenye mtandao wao wa klabu.

SIMBA KUTWAA UBINGWA NI NDOTO ZA ALINACHA

Image
Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Donald Ngoma, amesema hadi kumalizika kwa mzunguko wa kwanza Yanga itakuwa kileleni mwa msimamo wa ligi Kuu ya Tanzania Bara. Ngoma ameiambia YOUNGA AFRICAN, kuwa katika kipindi cha misimu miwili aliyocheza Tanzania anawajua vizuri wapinzani wao Simba hivyo haoni kama kuna tatizo kwa wao kuongoza ligi. “Ninauhakika hadi kumalizika kwa mzunguko wa kwnza Yanga tutakuwa kileleni au tunatofautiana pointi moja au mbili na timu itakayoongoza ligi kutokana na kasi tuliyonayo,” amesema Ngoma. Mshambuliaji huyo amesema siku zote Simba wamekuwa na papara ya kuanza kwa kasi lakini wao wamekuwa wazuri kwenye kumalizia mbio hizo na hatimaye kutwaa ubingwa. Amesema anatambua kuwa msimu huu ni mgumu na wenye ushindani mkubwa lakini haoni kikwazo ambazho kitaweza kuwazuia wasiweze kutwaa ubingwa. Ngoma tayari anabao moja alilofunga kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Lipuli ambapo timu hizo zilitoka sare ya 1-1.

KAMATI IMENITENDEA HAKI...

Image
Kiungo mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa ameachiwa huru na Kamati ya masaa 72 ambayo ipo chini ya Bodo ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara.    Kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia anayekipiga kwenye klabu ya Yanga Obrey Chirwa amesema anafurahi kwa kuachiwa huru na Kamati ya Nidhamu na Sheria ya TFF. Chirwa ameiambia SOKA DUNIANI , Kamati imetenda haki kwani yeye hakuhusika kabisa kwenye tukio lile lakini ni muda wake sasa kujipanga kwa ajili ya kuipigania timu yake kwenye mechi za ligi zinazoendelea. “Nashukuru kuona nimekutwa sina hatia kwasasa najipanga kwa ajili ya kuipigania timu yangu iweze kufanya vizuri kwenye ligi,”amesema Chirwa. Kwa pamoja, wakiwa wachezaji wa Yanga, Chirwa, Kaseke na winga mpya wa Difaa Hassan El- Jadida walidaiwa kumsukuma na kumwangusha refa Ludovic Charles katika mechi namba 236 ya Ligi Kuu iliyokutanisha timu hiyo na wenyeji, Mbao FC walioibuka na ushindi wa 1-0 Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Hata hivyo, ba...

MRITH WA BOSSOU ATUA JANGWANI

Image
Yanga inamsaka mrithi wa Vincent Bossou, ambaye aligoma kusaini mkataba mpya msimu ulioisha  Kwa mujibu wa gazeti la michezo la Mwanaspoti, Klabu ya Yanga imeanza mipango ya dirisha dogo la usajili baada ya kumvuta,  Kayembe Kanku Fiston kwa ajili ya majaribio,  akitokea klabu ya SM Sanga Balende yenye makazi yake nje ya Jiji la Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Beki huyo ameletwa na kiungo mpya wa Yanga, Papy Tshishimbi, Mcongo huyo amewahakikishia Yanga kwamba mchezaji huyo ni fundi na wataona yake kwenye majaribio ambayo atayaanza baada ya kocha kurejea. Amewaambia viongozi kuwa akishirikiana na kina Kelvin Yondani, Yanga itakuwa imara sana nyuma. Fiston atajaribiwa kwa wiki mbili ambapo endapo uwezo wake utakubalika, atasaini mkataba wa awali na Yanga na kurejea klabuni kwake. Imeelezwa kuwa atarejea tena nchini kuja kujiunga na mabingwa watetezi hao wa Ligi Kuu Bara wakati wa usajili wa dirisha dogo la usajili likalaofunguliwa Novem...