Young African inakuletea wachezaji wa kuchungwa kuelekea mchezo wa Yanga na Simba
Simba
na Yanga zitashuka dimbani siku ya Jumatano, Agosti 23 uwanja wa Taifa
Dar es salaam kwa ajili ya mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii
Ukiachana na historia ya pambano hilo, pia ukubwa wa mtanange huo unatokana na nyota wapya waliopo kwenye klabu zote mbili
Timu zote mbili zinatarajiwa kuwakosa nyota wake muhimu wa kikosi cha
kwanza kutokana na majeraha wanayouguza, Kakolanya, Mwashiuya na
Chirwa kwa upande wa Yanga wanatarajiwa kukosekana huku Bocco, Kapombe,
Mohammed Hussein kwa upande wa Simba wakiwa na asilimia kubwa ya kuukosa
mchezo huo.
YOUNG AFRICAN inakuletea wachezaji wa kuchungwa kuelekea mchezo wa Yanga na Simba
Amissi Tambwe - Yanga
Amekuwa
na rekodi nzuri ya kuifunga Simba tangu ajiunge na Yanga misimu 3
nyuma, Mrundi huyo anaitaji ulinzi mkubwa kumzuia hasa kwa mipira ya
hewani, kama kona na krosi
Shiza Kichuya - Simba
Ni mwiba kwa upande wa Yanga siku
ya Jumatano, mechi mbili za mwisho winga huyo aliibuka shujaa, safu ya
ulinzi ya Yanga inaitaji umakini mkubwa na kutoruhusu kufanya faulo
maeneo ya karibu kwani, Kichuya ni mpigaji wa mipra ya adhabu
Donald Ngoma - Yanga
Ni mshambuliaji mwenye kasi, nguvu
na jicho la goli, pia ni mzuri kwenye mashambulizi ya kushutukiza, ana
tazamiwa kuwa mwiba kwa Simba kama asipowekewa ulinzi dhabiti wa kumzuia
Emmanuel Okwi - Simba
Okwi ni mchezaji hatari sana kasi
yake, krosi murua na umakini wa kufunga amekuwa akiwapa tabu mabeki
wengi hivyo safu ya ulinzi ya Yanga inaitaji umakini wa kumdhibiti.
Thabani Kamusoko -- Yanga
Ndiye kiunganishi wa timu ya
Yanga, kuanzia safu ya ulinzi hadi ushambuliaji, hatakiwi kuwa huru
kufanya anachotaka kwani ndiye mwenye mipango yote ya klabu ya Yanga
Haruna Niyonzima - Simba
Amejiunga na Simba akitokea
Yanga, Harruna anatazamiwa kuwa mwiba kwa upande wa Yanga kama
asipowekewa ulinzi mkali, ni mchezaji mbunifu mwenye uwezo wa kufunga,
na kutengeneza nafasi kwa washambuliaji
Ibrahim Ajibu - Yanga
Siyo mshambuliaji wa kupewa nafasi
muda wote, Ajibu ni mmoja wa nyota wachache kwenye Ligi Kuu wenye uwezo
mkubwa wa kumiliki mpira kutokana na ubunifu wake mkubwa
Mzamiru Yassin - Simba
Ni mchezaji ambaye atamkwi sana,
ila ni mmoja wa nyota wa kuangaliwa sana kwani mechi nyingi ngumu kwa
upande wa Simba amekuwa ndiye msaada mkubwa sana
Comments
Post a Comment