LWANDAMINA AENDA KWAO ZAMBIA

Kocha wa Yanga George Lwandamina amerudi kwao Zambia leo baada ya kufiwa na mzazi wake wa kiume na atarudi nchini baada ya msiba kwisha 
 
Kocha wa klabu ya Yanga, George Lwandamina ameondoka Dar es Salaam kurudi kwao Zambia, kuhudhiria mazishi ya baba yake mzazi, aliyefariki dunia jana baada ya kusumbuliwa na maradhi ya Kiharusi.

Lwandamina ameiambia Goal, atakuwa huko hadi shuhuli za msiba zitakapo malizika ndipo atarudi Dar es Salaam kuendelea na kazi yake ya kukinoa kikosi cha Yanga.

 “Nakwenda nyumbani kwenye msiba wa Baba yangu baada ya kumaliza msiba nitarudi kazi kwa ajili ya kuiongoza Yanga kwenye michuano inayotukabili ya ligi ,”amesema Lwandamina.

Kocha huyo amesema baada ya yeye kuondoka majukumu yote ya timu amemuachia msaidizi wake Shedrack Nsajigwa pamoja akiamini anaweza kuwasimamia vizuri.

Amesema anatambua presha iliyopo baada ya kuanza na sare kwenye mechi yao ya kwanza msimu huu hivyo wanajipanga kuhakikisha wanafanya vizuri na kutwaa kutetea ubingwa wao.

Yanga kwasasa inashika nafasi 10 kwenye msimamo ikiwa na pointi moja baada ya kulazimishwa sare ya kufungana mabao 1-1 na Lipuli ya Iringa.

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA ILIVYONUSURIKA KUSHUKA DARAJA MWAKA 1989

TUJIKUMBUSHE MECHI KALI KATI YA YANGA NA SIMBA NYAMAGANA 1974?

JINSI YANGA ILIVYOIADHIBU SIMBA MWAKA 1994