SARE KITU GANI? SUBIRI MZIKI WETU

Kocha wa Yanga amesisitiza kuwa Yanga bado ipo imara na malengo hayajavurugika ingawa Lipuli walikamia mchezo 
Kocha wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara George Lwandamina amesema sare waliyoipata jana dhidi ya Lipuli FC haijawavurugia mipango ya kutetea ubingwa wao.
Lwandamina ameiambia SOKA DUNIANI timu yake ilicheza vizuri lakini wapinzani wao waliziba njia walizopanga kuzitumia ndiyo mana wakapata sare.

"Tulicheza vizuri wachezaji walijituma lakini tukashindwa kutumia nafasi tulizozipata lakini hilo halitutoi kwenye mbio za ubingwa kwasababu ndiyo mchezo wa kwanza bado tuna michezo mingi," amesema.

Mzambia huyo amesema kuwa wapinzani wao waliingia kwa kuwakamia na kuwachezea rafu baadhi ya wachezaji wake kitu ambacho kilivuruga mipango yao.

Amesema wanetambua mapungufu yao na wanakwenda kuyafanyia kazi akiamini kwamba mchezo unaofuata dhidi ya Njombe Mji watarekebisha na kupata matokeo.

Yanga ilianza vibaya harakati za kutetea ubingwa wake msimu huu baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo uliochezwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA ILIVYONUSURIKA KUSHUKA DARAJA MWAKA 1989

TUJIKUMBUSHE MECHI KALI KATI YA YANGA NA SIMBA NYAMAGANA 1974?

JINSI YANGA ILIVYOIADHIBU SIMBA MWAKA 1994