KAMUSOKO SI WA KAWAIDA;;;;HAJI MANARA

Kwa mujibu wa Haji Manara ana amini kwa uwezo mkubwa alionao Thabani Kamusoko si wakucheza hapa 
 
Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amemvulia kofia kiungo wa klabu ya Yanga Mzimbabwe, Thabani Kamusoko kutokana na umahiri wake mkubwa wa kusukuma kabumbu.

Thabani Kamusoko alijiunga na Yanga misimu miwili nyuma akitokea klabu ya FC Platnumz ya nchini Zimbabwe.

Katika misimu mitatu Jangwani, Kamusoko amefanikiwa kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu Bara, moja la FA na Ngao ya Jamii, kadhalika na kuiwezesha Yanga kucheza hatua ya makundi, kombe la Shirikisho Afrika misimu miwili nyuma chini ya mwalimu, Hans Van Pluijm.

Akitumia akaunti yake ya Instagram, Haji Manara amesema kiungo huyo si wakucheza nchini hapa kutokana na uwezo wake mkubwa

"Huwa sifichi mahaba yangu kwa mchezaji anayenivutia uwanjani, hata kama anachezea Klabu nisiyoishabikia, Scara kamusoko hapewi heshma anayostahili nchi hii, ni level ya kucheza Europe"

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA ILIVYONUSURIKA KUSHUKA DARAJA MWAKA 1989

TUJIKUMBUSHE MECHI KALI KATI YA YANGA NA SIMBA NYAMAGANA 1974?

JINSI YANGA ILIVYOIADHIBU SIMBA MWAKA 1994