NGOMA APANIA KUIFUNGA SIMBA KESHO
Ngoma ameiambia YOUNGA AFRICAN, haoni ugumu wowote kuelekea mchezo huo na hiyo ni kutokana na kupona majeruhi yaliyomsumbua kwa muda mrefu na ubora wa kikosi chao ulivyo.
“Bado sijaona beki wa Simba ambaye anaweza kunizuia kwanza nina hasira nao sana baada ya kukosa mechi mbili za msimu uliopita imeniuma sana walivyotufunga na nisingependa matokeo yale yajirudie tena,”amesema Ngoma.
Mshambuliaji huyo aliyeongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuichezea Yanga, amesema anataka kurudisha heshima Yanga kama ilivyokuwa wakati wa nyuma ambapo waliweza kutamba kwa kuzifunga timu zote kubwa nchini.
Amesema ili kuthibitisha kuwa wao ni timu kubwa nilazima waifunge Simba kesho ili kujiweka katika mazingira mazuri hata ya kutetea taji lao la ligi ya Vodacom Tanzania Bara.
Ngoma ameifunga Simba mara moja tangu alipotua nchini misimu miwili iliyopita akitokea FC Platinum ya kwao Zimbabwe sambamba na kiungo mkongwe Thabani Scara Kamusoko.
Comments
Post a Comment