Cannavaro aipa Yanga ushindi dhidi ya Kagera Sugar


Mabingwa watetezi Yanga Oktoba 14 watakuwa ugenini uwanja wa Kaitaba kucheza na Kagera Sugar na nahodha wake Cannavaro ameahidi ushindi 
 
Nahodha mkuu wa klabu ya Yanga Nadir Haroub ‘Cannavaro, amesema wamejipanga kucheza kwa bidii ili kuweza kushinda mechi yao dhidi ya Kagera Sugar.
Cannavaro, ameiambia YOUNGA , wamefanya mazoezi ya kutosha kujiandaa na mechi za kanda ya ziwa na anaamini watashinda kutokana na uimara.

“Nashukuru mambo yetu yote yanakwenda vizuri lengo letu ni ushindi na ninamaani hivyo kulingana na matayarisho yetu,” amesmea Cannavaro.

Cannavaro ambaye hajaichezea Yanga hata mechi moja amesema hamasa ni kubwa kwenye kambi yao.

Nahodha huyo amesema pamoja na ligi kuonekana kuwa mgumu lakini  wamejipanga kufanya kama msimu uliopita.

Yanga inashika nafasi ya sita kwenye msimamo ikiwa na pointi 2 ambazo ndiyo wanazo kwasasa baada ya kucheza mechi tano za ligi.

Comments

Popular posts from this blog

SIMBA ILIVYONUSURIKA KUSHUKA DARAJA MWAKA 1989

TUJIKUMBUSHE MECHI KALI KATI YA YANGA NA SIMBA NYAMAGANA 1974?

JINSI YANGA ILIVYOIADHIBU SIMBA MWAKA 1994